Friday, December 6, 2013

Hivi ndivyo Zuma alivyotangaza kifo cha Mandela...

Mandela

"My Fellow South Africans, our beloved Nelson Rolihlahla Mandela, the founding President of our democratic nation, has departed.

He passed on peacefully in the company of his family around 20h50 on the 5th of December 2013. He is now resting. He is now at peace. Our nation has lost its greatest son. Our people have lost a father.

 "Although we knew that this day would come, nothing can diminish our sense of a profound and enduring loss. His tireless struggle for freedom earned him the respect of the world.

"His humility, his compassion, and his humanity earned him their love. Our thoughts and prayers are with the Mandela family. To them we owe a debt of gratitude. They have sacrificed much and endured much so that our people could be free.

"Our thoughts are with his wife Mrs Graca Machel, his former wife Ms Winnie Madikizela-Mandela, with his children, his grand-children, his great grand-children and the entire family. Our thoughts are with his friends, comrades and colleagues who fought alongside Madiba over the course of a lifetime of struggle. 

"This is the moment of our deepest sorrow. Our nation has lost its greatest son. Yet, what made Nelson Mandela great was precisely what made him human. We saw in him what we seek in ourselves. And in him we saw so much of ourselves.

"Fellow South Africans, Nelson Mandela brought us together, and it is together that we will bid him farewell. Our beloved Madiba will be accorded a state funeral. I have ordered that all flags of the Republic of South Africa be lowered to half-mast from tomorrow, 6 December, and to remain at half-mast until after the funeral.  
 "This is indeed the moment of our deepest sorrow. Yet it must also be the moment of our greatest determination. A determination to live as Madiba has lived, to strive as Madiba has strived and to not rest until we have realized his vision of a truly united South Africa, a peaceful and prosperous Africa, and a better world.
"We will always love you Madiba! May your soul rest in peace. God Bless Africa. Nkosi Sikelel' iAfrika." 
enzi za uhai wake akiwa na Mama Winnie Mandela
 


Friday, November 15, 2013

MBUNGE KAPUYA YAMKUTA YA UBAKAJI NA KUTISHIA KUUA


Mbunge wa Urambo Magharibi, Profesa Juma Kapuya (CCM).MBUNGE wa Urambo Magharibi, Profesa Juma Kapuya (CCM), ameingia katika matata. Katika kujaribu kudhibiti mtoto wa shule ambaye anadai alibakwa naye na kuambukiwa virusi vya ukimwi, mbunge huyo ametoa vitisho vya kuua mtoto huyo na kujiua kama njia ya kuepuka dhahama inayoelekea kumkabili.

Siku moja baada ya gazeti hili kuripoti habari za mbunge mmoja (bila kumtaja jina), jana asubuhi Profesa Kapuya ameibuka na kumtisha mwanafunzi huyo mwenye miaka 16 anayesoma Shule ya Sekondari Turiani iliyoko Magomeni jijini Dar es Salaam.

Baada ya kujua kuwa mtoto huyo ndiye alitoa habari za masahibu hayo, ambayo mbunge hakutaka yajulikane, alimpigia simu mtoto huyo, na baadaye kutuma meseji kadhaa za vitisho.

Jana Tanzania Daima ilishuhudia baadhi ya meseji za simu zilizotumwa na Profesa Kapuya kwenda kwa mtoto huyo.

Alfajiri saa 11:21 kupitia simu yake ya mkononi yenye namba 0784993930, Profesa Kapuya alituma ujumbe ufuatao kwa mtoto huyo: “chagueni kunisubiri tuje tuongee au mnataka kufa?”

Baadaye saa 1:07 asubuhi, alituma ujumbe mwingine kutoka simu hiyo hiyo kwenda kwa mtoto huyo, ukisema: “Mkiuawa, itakuwa nzuri, itawapunguzia gharama za kuishi. Usitake kugombana na serikali, mtoto mdogo kama wewe. Sisi ndo wenye nchi yetu.

“Mwambieni Mbowe mwenye hilo gazeti awape nyumba ya kuishi. Si mmemuingizia hela leo? Mnatumika bure watu wanaingiza hela nyingi, mmenitibua lazima niwauwe wiki hiii haitaisha, nitapanga kambi popote.

“Jana si wamekuficha? Tuone kama utalindwa milele. Kazi ya kulindwa imeisha, maana wameshatengeneza hela. Lazima mvae sanda. Hilo sio ombi, ni wajibu wenu. Mnajitia mafia watoto sio? Watoto wetu wanauza unga, nani anawakamata? Nani atapigana nasi?”

Hata hivyo, baada ya kuhisi kuwa watoto hao wamedhamiria kumchukulia hatua, na wamewasiliana na taasisi mbalimbali za kiraia na serikali zenye uwezo wa kumtia adabu, mbunge huyo alimtumia mtoto huyo ujumbe wa kuonyesha alikuwa anafikiria kunywa sumu..

Ujumbe huo uliotumwa kwa mtoto huyo saa 11:2 3 ulisema: “nimwakosea sana, acha nife mie nakunywa sumu nijiue, na nyie mje mnizike.”

Hasira za Profesa Kapuya dhidi ya mtoto hao zilitokana na hatua ya mtoto huyo na dada yake kufichua unyama wanaodai kutendewa na mbunge huyo, ambaye amewahi kushika nyadhifa kadhaa za uwaziri katika Serikali ya Awamu ya Nne.

Tangu alipogundua kuwa mtoto huyo alizungumza na gazeti hili juzi, saa 5:17 usiku wa kuamkia jana alituma ujumbe usemao: “Si mpo Bilz? Sasa tupo pamoja na nyie mpaka usiku.”

Baadaye saa 5:31 alituma ujumbe  huu: “Hivi hamkubali kushindwa? Leo ulifuata nini ofisi ya CCM?”

Ujumbe huo ulitokana na ukweli kwamba dada wa mtoto anayedaiwa kubakwa alifika Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) juzi asubuhi kuonana na Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana, ili kuomba chama kimsaidie kumbana Profesa Kapuya, ambaye alikuwa ameanza kuwatisha yeye na mdogo wake.

Hata hivyo, kwa mujibu wa mtoto huyo, Kinana alisema suala hilo si la chama bali la Profesa Kapuya binafsi.

Mtoto huyo alikataa ushauri wa kupeleka shauri hilo mbele ya vyombo vya sheria, akidai kuwa jitihada zake zimekuwa zinazimwa na mbunge huyo anayedai serikali haiwezi kumfanya lolote.

Alisisitiza kuwa hana imani na serikali, lakini akasema yupo tayari kuchukua hatua kali dhidi ya Profesa Kapuya iwapo atasimamiwa na watetezi wa haki za binadamu.

Baadhi ya mashirika yanayotetea makundi kadhaa yakiwamo Kituo cha Sheria na Haki za BInadamu (LHRC) na Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP) yalijitokeza kumsaidia watoto hao, ambao ni yatima.

Mtoto huyo na dada yake, wakizungumza na gazeti hili kwa hofu mafichoni, walisema kwa sasa hawana imani tena kama kuna serikali nchini Tanzania kwa kuwa wamedhalilishwa, wametembezwa hadi Bungeni na wabunge bila hatua kuchukuliwa, licha ya kutoa taarifa katika kituo cha polisi Oysterbay tangu mwaka jana.

Hata hivyo, kabla ya tukio la watoto hao kuripoti, ofisi za gazeti hili juzi usiku kulikuwa na watu waliokuja wakiwatafuta watoto hao, huku wakiwatisha kwa simu na kuwatolea maneno ya kejeli, wakidai watawamwagia tindikali.

Mmoja wa watoto hao, alidai kuwa miongoni mwa vijana waliokuwa wanawatisha juzi walikuwa katika gari T170 BGY, Benz, Cream Metalic, ambayo inamilikiwa na mbaya wao.

Jana gazeti  hili lilichapisha habari kuwa  mwanafunzi huyo aliyesema kuwa waziri huyo  alimbaka kwenye hoteli moja ya kitalii iliyoko jijini Dar es Salaam mwaka 2011, na kurudia tena kitendo hicho katika Jengo la Biashara Complex lililoko Mwananyamala Juni 3, 2012 alipoitwa kwenda kuchua ada kwa mara ya pili. 

Akizungumza kwa uchungu, alisema mbunge huyo alifanya kitendo hicho kwenye Hoteli ya Giraffe, Jijini Dar es Salaam mwaka 2011.

Alisema kuwa yeye alikuwa na urafiki na mwanafunzi mwenzake Zuhura Mwaking’inda. Mwaking’inda amewahi kuwa Diwani wa Kata ya Sinza Jimbo la Ubungo, Jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa mwanafunzi huyo, rafiki yake (mtoto wa Mwaking’ida) alikuwa amepooza hivyo alikuwa analazimika kumhudumia hali iliyowaunganisha hadi huyo mtoto alipochukua jukumu la kumtambulisha kwa baba yake ambaye naye alimtambulisha kwa Kapuya ili aweze kumsaidia fedha kwa jili ada.

Mwanafunzi huyo alisema baada ya kutambulishwa aliitwa katika hoteli moja jijini Dar ambapo baada ya kufika mapokezi wafanyakazi wa  hoteli hiyo walimkataza kuingia chumbani katika maana kwamba umri wake alikuwa mdogo (mwaka 2011 alikuwa na miaka 14), lakini Kapuya aliamrisha aje chumbani pamoja na dereva na kumwingiza kwa nguvu.

Akiwa chumbani alimlazimisha kulala naye kisha kumpa sh laki saba, badala ya sh elfu sitini na saba kiasi ambacho kilikuwa ndio mahitaji halisi ya ada.

Mwanafunzi huyo amesema baada ya muhula mmoja aliitwa tena na mbunge huyo katika Jengo la Biashara Complex lililoko Mwananyamala tarehe 3 June 2012, ambapo pia alimlazimisha kulala naye kwenye zulia la ofisi yake, kisha kumpa sh 350,000/.

Alisimulia kwamba wakati anatoka kwa huzuni ofisini kwa mbunge huyo, mmoja wa wahudumu wa hapo alimuuliza kwanini anatoka kwa huzuni, alimweleza kisa hicho, na huyo mama aliangua kilio kwa kumwambia “mwanangu umekufa pole tu, huyu baba ni muathirika wa ukimwi”.

Aliongeza kuwa baada ya kuambiwa vile alilia na kufanya fujo hapo mapokezi hadi alipokamatwa na walinzi wa kisha kupelekwa kituo cha polisi kufunguliwa mashtaka, lakini akiwa polisi alipoeleza mkasa wote, Polisi walilazimika kumwita Kapuya na wakawasuluhisha kwa makubaliano kwamba Kapuya atakuwa anamlipia ada, na kumpa pesa za matumizi sh. laki tatu kila mwezi, jambo ambalo amekuwa akilitekeleza kupitia simu yake ya mkononi 0755993930.

Kwa mujibu wa mwanafunzi huyo, 24 Januari 2013, alifika mtu nyumbani kwao mtu mmoja (jina tunalihifadhi) na kujitambulisha kuwa yeye ni jambazi na kuwa alitumwa kwenda kuwaua kwa malipo ya sh. milioni 50, lakini alipokuta ni watoto wadogo aliwasamehe, na kusema yeye ni jambazi sugu hawezi kupoteza nguvu zake kuua vitoto.

Alienda akiwa na bastola, maji kwenye chupa yanayodhaniwa kuwa ni tindikali na bomba la sindano. Kwa mujibu wa mtoto huyo, jambazi huyo anasema kuwa tayari alilipwa milioni 15 za awali.

Mtoto huyo alisema jambazi huyo aliwambia kuwa yeye ni rafiki wa mtoto wa Kapuya na wanamfahamu vizuri, lakini hataweza kuaua baada ya kubaini kuwa wao ni yatima tu.

Hata hivyo kufikia mwezi Februari mwaka huu, mtu asiyefahamika alienda nyumbani na kutelekeza gari aina ya T.199 BGY Mercedes Benzi ya Blue wakati wanafunzi hao wakiwa shuleni, kisha kuacha ufunguo kwa jirani yao kwa maelekezo kuwa wakifika awapatie.

Na Kapuya aliwapigia simu kuwaarifu kuwa amempa zawadi ya gari kwa ajili ya matumizi ila yeye na dada yake wanaruhusiwa kuuza ili wapate pesa kwa ajili ya mahitaji yake siku zilizosalia, kwani muda sio mrefu baada ya uchguzi mkuu 2015, Kapuya atakuwa Waziri Mkuu, hivyo itakuwa ngumu yeye kumtumia huyo binti pesa kama alivyoelekezwa na jeshi la polisi kituo cha Oysterbay.

Baada ya mwanafunzi huyo na dada yake ambaye ana umri wa miaka 20, kupewa gari walishindwa kulitumia hivyo kutoa taarifa polisi kwani kwa kupokea gari hilo  ilikuwa ni kuwatelekeza kwani yeye hana hata hela ya kuweka mafuta ya gari, hivyo walienda polisi ili kesi ipelekwe mahakamani kumshtaki kapuya.

Polisi wa Oysterbay walikubali kulipeleka tatizo hilo kwa Katibu wa Bunge, ambaye alimwita mwanafunzi huyo na mdogo wake waende Dodoma kukutana na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ingawa walipofika Dodoma walikaa na kamati ya hiyo kwa maelezo kuwa Kapuya hakuwepo hadi Bunge lilipoisha walirejeshwa Dar es Salaam.

Mtoto huyo na dada yake alitoka ofisi za CCM lakini akiwa anaelekea kituo cha basi alithadharishwa na mwanafunzi mwingine kwa haraka kuwa akimbie kwa kuwa atamwagiwa tindikali na watu waliokuwa wanamfuata nyuma, alikimbilia katika mtaa wa Hoteli ya Star light kisha aliomba msaada baada ya kupotea njia na hivyo alisaidiwa na mama mmoja kufikishwa chumba cha habari cha Channel Ten.

Ni katika chumba hicho ndio mwandishi wa habari hizi alienda na kuwakuta watu wawili hao waliokuwa wanamhitaji binti huyo lakini walikatazwa kumchukua.
-TANZANIA DAIMA

Siku mtoto wangu alipopata Kipaimara

 

Carrenflora Mgonja wa kundi la wajasiliamali wa kikundi cha Habari Group akiwa na mumewe Patson Mlandali wakati wa kumfanyia part ya kipaimara bint yao Elizabet iliyofanyika katika ukumbi wa Abiola Buza Dar es salaam jana
Washereheshaji wa shughuli hiyo Anti Latifa kushoto na Sakina Lioka wakiwa na CArren Mgonja wakati wa sherehe ya mwanae
Elizabet
kutoka kushoto Hellen Mwango na Somoe N,gitu wafanyakazi wenzie
WAZAZI WAKICHEZA MZIKII
WAZAZI WAKITOA NENO LA KUWAKARIBISHA WAGENI

picha zaidi zinakuja
Carrenflora Mgonja  

Friday, August 23, 2013

ANGELLAH KAIRUKI ALIPOTOA BAISKELI KWA WATOTO WENYE ULEMAVU WA VIUNGO



Angella Kairuki akiwa na watoto wake Kemy pamoja na Esta muda mfupi baada ya kukabidhi baiskeli hizo.
Mama kairuki akiongea na mtoto Halima ambaye naye pia alipata baiskeli hiyo.
Wazazi wakiwa na watoto wao baada ya kukabidhiwa baiskeli zao

..........

...............

mtoto mmojawapo wa Mama Kairuki akimuendesha mtoto mmoja wapo aliyekabidhiwa baikeli

Mama Kairuki akiwa na familia yake pamoja na mtoto Halima
Mama Kairuki akisisitiza jambo

Mama Kairukia akimuendesha mtoto Halima





Mheshimiwa akikabidhi  baadhi ya zawadi zingine kwa mzazi kwa niaba ya watoto

Mama yake na Zitto Kabwe ambaye pia ni kiongozi wa SHIVYAWATA akishukuru kwa niaba ya uongozi mzima wa chama hicho
Mtoto akifurahia zawadi zake


WAZIRI KAIRUKI ATOA MSAADA KWA WATOTO WENYE ULEMAVU

NAIBU Waziri wa Katiba na Sheria, Angellah Kairuki ambaye pia ni Mlezi Mkuu wa kikundi cha waandishi wa habari wajasiriamali (HABARI GROUP), ametoa msaada wa basikeli maalum kwa watoto wenye ulemavu kupitia shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu nchini (SHIVYAWATA).

Angellah alikabidhi viti hivyo jana, vyenye thamani ya zaidi ya sh. milioni 12, kwa baadhi ya watoto hao, na baadaye kuwafikia watoto wote wenye mahitaji.

Akizungumza wakati wa kukabidhi, alisema viti hivyo ni maalum kwa watoto wenye miaka kuanzia sifuri hadi tisa, na ametoa kutokana na kuguswa na matatizo ya wenye ulemavu na pale anapopata nafasi anawakumbuka.

"Nimekuwa nikifanya kazi zaidi na watoto wenye ulemavu wa kusikia (Viziwi), lakini pia nikaona kuna kundi lina mahitaji zaidi, hivyo kwa kidogo nilichopata  nikawambuka, nafanya kazi kwa kushirikisha familia yangu,  sitaishia hapa nitawasaidia zaidi kwa kadri nitakavyojaaliwa,"aliongeza kiongozi huyo aliyekuwa ameambatana na wanaye wawili.

Akishukuru kwa msaada huo, Katibu wa SHIVYAWATA, Felician Mkudem alisema kuwa  wanafarijika sana kuona watu muhimu kama Angellah, wanakumbuka na kuwajali.

"Kiongozi wa serikali ndiye jicho na sauti za watu wenye ulemavu, hivyo kwa kutusaidia vifaa saidizi kwa wtaoto wenye ulemavu ni faraja kubwa sana, kwani mambo hayo ni miongoni mwa tunayoyapigania,"alisema.

Mkude alitumia fursa hiyi kukamabidhi nyaraka mbalimbali, ikiwemo mpango mkakati wa ukondaishaji wa watu wenye ulemavu na sheria mbalimbali zinazowahusu.
Mwenyekiti wa Chama cha Watu wenye Ulemavu wa Viungo, (CHAWATA), Shida Salum aliishukuru serikali ya Rais Kikwete kuwakumbuka watu wenye ulemavu na kuwafanyia mengi kwa ajili ya ustawi wao.

Wazazi wa watoto hao walishukuru kwa msaada huo na kwamba utawasaidia  watoto wanaosoma waliokuwa wanabebwa kwenda na kurudi shule, na wengine waliokuwa hawajaanza masomo kutokana na hali ngumu ya kuwafikisha shuleni.

Viti hivyo vipatavyo 29, viligawiwa kwa watoto watano, wengine wawili wakiwa wanapata huduma katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na vingine vilivyobaki watatafutwa wenye mahitaji na kukabidhiwa.

Thursday, July 25, 2013

Dk. Mwakyembe awagwaya washirika dawa za kulevya

Dk Mwakyembe
 Katika hali ya kushangaza, Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, amepata kigugumizi cha kuwachukulia hatua maofisa wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) walioruhusu shehena kubwa ya dawa za kulevya kupita hadi Afrika Kusini.
Ni takribani wiki ya tatu sasa tangu wasichana wawili wa Tanzania walipokamatwa na kilo 150 za dawa za kulevya aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 6.8 nchini Afrika Kusini wakati zikisafirishwa kutoka Tanzania.
Jana NIPASHE lilizu ngumza na Dk. Mwakyembe kwa njia ya simu kutoka Kagera, lakini alijibu kwamba, hana taarifa za kina kuhusu sakata hilo.
Hata hivyo, alisema yeye hausiki nalo kwa kuwa suala la uhalifu linaihusu Polisi na kumwelekeza mwandishi awasiliane na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi au Jeshi la Polisi.
Taarifa za kukamatwa kwa wasichana hao nchini Afrika Kusini zilipatikana Julai 5, mwaka huu.   Walikamatwa na maofisa wa Mamlaka ya Mapato ya nchi hiyo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo, uliopo eneo la Kempton Park.
 Taarifa hiyo ilionyesha wasichana hao walisafirisha dawa hizo kupitia ndege ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini.
Waliokamatwa hivi karibuni ni Agnes Jerald (25), Melisa Edward (24), ambao wameshtakiwa Afrika Kusini.
Hata hivyo, kigugumizi cha viongozi hawa na hususan cha Waziri Mwakyembe, kinaibua maswali mengi, ambayo yanaashiria kwamba, biashara haramu ya dawa za kulevya itakuwa inahusisha mtandao wa watu wenye nguvu nchini.
Itakumbukwa kwamba, ni Mwakyembe huyu huyu, ambaye aliifumua Mamlaka ya Bandari (TPA), kwa kuwatimua kazi wakurugenzi wakuu pamoja na kutengua uteuzi wa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi kutokana na utendaji usio na tija na hasa baada ya kutokea kwa wizi wa shaba bandarini.
Wizi huo ulitokea usiku wa kuamkia Septemba 8, mwaka jana jambo, ambalo lilimkasirisha Waziri Mwakyembe.
Alifanya ziara bandarini hapo na kuagiza watu wote waliohusika na wizi huo kukamatwa na kufunguliwa mashitaka.
Pia Juni 12, mwaka jana,  Mwakyembe baada ya kuwang’oa vigogo wanne wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), alisafiri kwa treni kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma ili kujionea utendaji kazi wa shirika hilo.  Mara baada ya kuwasili katika Stesheni ya Dodoma saa 1:30 asubuhi,  alizungumza na waandishi wa habari na kusema akiwa katika safari hiyo, alipata fursa za kutembelea mabehewa yote na kuzungumza na abiria. Alisema alibaini hujuma nzito katika Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), ikiwamo ofisa mmoja kuwaibia abiria kwa kughushi viwango vya nauli na hivyo akaagiza afukuzwe kazi.
Licha ya kuagiza kutimuliwa kwa ofisa huyo, pia alitangaza kuandaliwa utaratibu wa kufanya mabadiliko kadhaa katika kuboresha usafiri huo, ikiwamo kuondoa malipo ya nusu nauli kwa watoto wadogo kuanzia miaka mitatu hadi miaka 10 na pia kuondolewa kwa utaratibu wa malipo ya mizigo midogo ya abiria.
Takwimu zinaonyesha kumekuwa na wimbi kubwa la Watanzania wanaojiingiza katika biashara haramu ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi na kwamba, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, watuhumiwa 10,799 walikamatwa kwa kujihusisha na dawa hizo.
Katika kipindi hicho, Watanzania 240 walikamatwa katika nchi za Brazil, Pakistan na Afrika Kusini, kuharibu taswira ya nchi na kusababisha Watanzania wasio na hatia kupata usumbufu na masharti magumu wanapotaka kusafiri kwenda nchi mbalimbali duniani.

chanzo...gazeti la nipashe