Thursday, April 18, 2013

MAELFU WAHUDURIA MAZIKO YA MAREHEMU BI KIDUDE.




Tulikupenda lakini Mungu amekupenda zaidi R.I.P..........KIDUDE BINTI BARAKA

Jeneza la bibi likielekea msikiti kwa ajili ya kusaliwa

Mtangazaji Hassan Bond, Fid Q, Diamond Platnumz na Ruge Mutahaba wakiwa msibani nyumbani kwamarehemu bi Kidude, Zanzibar

Msanii Fid Q, Baraka cousin ya Marehemu Bi Kidude na Hassan Bond Mussa (FID Q ndo alikuwa msanii wa kwanza mkubwa kufika msibani kwa bibi)

Ruge mutahaba, Babu Tale and Guru. .......msibani kwa Bi Kidude

Guru G na Mh Bhaa mazikoni

Hassan na Fid Q wakiwa katika picha ya pamoja na familia ya Marehemu Bi Kidude

Sehemu ya umati wa Watu waliofika msibani

Endelea kuwa nasi kwa tukio zima la maziko ya Bibi yetu
picha kwa hisani ya Tanzania One.

Wednesday, April 17, 2013

Bi Kidude afariki dunia....

marehemu Bi Kidude
MWIMBAJI nguli wa muziki wa taarabu na mkongwe kuliko wote, Fatuma Binti Baraka Bi Kidude amefariki Dunia leo mjini Zanzibar.
  1. Mwanamuziki mkongwe katika Taarab Fatuma Bint Mbaraka maarufu kwa jina la Bi Kidude amefariki dunia leo mchana  huko Bububu Zanzibar, sehemu alikokuwa anaugulia kwa kipindi sasa.
  2. Mwili wake utahamishiwa kwake Rahaleo na mazishi yatakuwa kesho. 
  3. Bi Kidude alizaliwa katika kijiji cha Mfagimaringo..Alikuwa binti... wa mchuuzi wa nazi naA hakuna anayejua haswa Bibi huyu alizaliwa tarehe ngapi, kuna hata mawazo kuwa alikwishafikisha miaka 102. 
  4. Katika mwaka 1920 tayari alikuwa amekwisha anza kuimba katika vikundi vya sanaa kule kwao...mwaka 1930 alijiunga na Egyptian Musical Club ya Dar es Salaam na kuzunguka miji mingi ya Tanganyika wakati ule .....
  5. Mwaka 1940 alirudi Zanzibar ambako awali alikuwa amekimbia kwa kuwa aliozwa kwa nguvu na mtu aliyemzidi sana umri.
  6. Bi Kidude pia liwahi kuimba na Sitti Binti Sadi wakati wa ujana wake, na katika maisha yake Bi Kidude amekwisha zunguka mabara yote akiimba katika majukwaa na wanamuziki maarufu ulimwenguni

Tuesday, April 16, 2013

JOKATE AMCHEKA UWOYA

MWANAMITINDO Jokate Mwegelo ‘Kidoti’, ameangua kicheko baada ya kusikia mwigizaji Irene Uwoya kunaswa hotelini na Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Jokate Mwegelo ‘Kidoti’.
Jokate aliangua kicheko hicho juzikati jijini, Dar wakati alipozungumza na paparazi wetu na alipogusiwa kuhusu suala la Uwoya kunaswa na Diamond, alicheka sana huku akimshangaa.
“Hahaha sasa ndiyo nini tena, yeye si aliwahi kunisema mimi nakwapua mabwana? Sasa leo imetokea kwake tena!” alisema Jokate.


Irene Uwoya.
Chanzo:www.globalpublishers.info

Monday, April 15, 2013

NDEGE YAANGUKA JIJINI ARUSHA NA KUUA MTU MMOJA

Habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba ndege iliyokuwa inamilikiwa na Wakili maarufu Marehemu Nyaga Mawala aliyefariki wiki 3 zilizopita na kuzikwa huko Nairobi imeanguka ikiwa katika hatua za mwisho za kutua  katika kiwanja cha ndege cha arusha.

Taarifa zinasema kuwa ndege hiyo ilikuwa na rubani pekee anayejulikana kwa jina la Jamal B S, au maarufu kama Bob Sambeke aliyekuwa anatokea West Kilimanjaro.


Taarifa zaidi zinasema kuwa  rubani huyo   amefariki  muda  mfupi  baada  ya  ajali  hiyo  kutokea  na   mwili  wake  umekimbizwa   hospitali ya Mount Meru
...

Maelezo zaidi kuhusu ajali hiyo ni kwamba ndege hiyo ilijaribu kutua baada ya masaa ya kawaida ya kufunga kiwanja(saa 12.30jioni) kupita.


Kiwanja cha ndege cha Arusha hakina taa za AGL, hivyo huwa kinamaliza au kufunga shughuli zake saa 12.30 za jioni, na hivyo kina'operate kwa masaa 12 tu.Na kawaida ma'controller huondoka baada ya closure ya kiwanja..

Mungu  ailaze  mahali  pema  roho  ya  marehemu
...
Picha ya ndege iliyoanguka
Name:  DSC03435.JPG
Views: 0
Size:  7.26 MB


Name:  DSC03444.JPG
Views: 0
Size:  6.98 MB
Eneo ambalo ndege iliyoanguka, kutoka eneo hilo mpaka landing truck ni kama 1km. Mbele ya mabaki hayo ya ndege kuna mti mmoja ambao unasadikiwa kuwa  ndege hiyo ilijigonga na kudondoka chini.

Wednesday, April 10, 2013

YALIYOJIRI KATIKA SIKU YA KANUMBA....



MAMA KANUMBA AKISHUKURU WATANZANIA
JACQULINE WOLPER NAE ALIZUNDUA MOVIE YAKE UCIKU HUU
MGENI RASMI ALIKUWA MEYA WA KINONDONI
marafiki kutona Ghana walikuwepo
kulitolewa tuzo na moja wapo ilienda kwa Millard Ayo #fellowblogger na mtangazaji wa Amplifire Cloudsfm
Hongera mtu wangu wa nguvu









                                   Miriam Odemba alihudhuria pia











 



mashabiki wake walijitokeza kwa wingi.......bye 8020fashion.





Duh hili pozi la Partck Mwilongo na Carren Cyprian ni full balaa....

Waandishi waandamizi Tanzania wenye uwezo wa kusimama sehemu zote, michezo, burudani, siasa na biashara wakiwa wamepozi walipokutwa na kamera ya Handeni Kwetu mwishoni mwa wiki maeneo ya Leaders Club.
Kushoto anaitwa Patrick Mwilongo mwenye maskani yake mjini Bagamoyo akiiwakilisha New Habari 2006 kwa magazeti ya Mtanzania, Bingwa, Dimba, Rai na The African, wakati Carren Cyprian anayeandikia Gazeti la Nipashe. Hili lilikuwa pozi la aina yake.... Duh..haaaaaaaa......

from Handeni Kwetu

Friday, April 5, 2013

Habari Group wapewa somoooo

Mwenyekiti akifungua kikaooooo

mama akisisitiza jambo kwa mwanachama mpya wa Habari Group...
mama, dada na mwalimu wakiwasikiliza ndugu zao...
na mimi na pozi languuu

mtu na dada yake jamani haoooo....mmmh

haaaaaaa........
NAIBU Waziri wa Sheria na Katiba, Angellah Kairuki amewataka wanachama wa kikundi cha waandishi wa habari cha kujikomboa kiuchumi (Habari Group) kupendana na kuaminiana ili kukifikisha
kikundi hicho mbali.
Kairuki ambaye pia ni mlezi wa Habari Group, alikitaka kikundi hicho kutokuwa wachoyo wa kusaidia waandishi wa habari wengine wenye nia ya kuungana na kufanikiwa kimaisha.
 Akizungumza na kikundi hicho Dar es Salaam juzi, alisema ili mtu afanikiwe ni lazima awe mwenye upendo na kusaidia wengine pale penye mwanya wa kufanya hivyo na kuwataka wanachama wote kuwa na
moyo wa kujitolea kwa ajili ya kikundi.
"Sitopenda kusikia kikundi hiki kimekufa kwa sababu ya mifarakano na chuki miongoni mwenu kwani kwa kufanya hivyo hamtofikia malengo mliyokusudia," alisema Kairuki.
Aliongeza kuwa wakati anaingia madarakani aliweka vipaumbele kwa wafanyakazi wa majumbani, madereva wa aina zote, wafanyakazi wa mashambani, wahudumu wa baa na nyumba za wageni, walinzi na
waandishi wa habari.
Na kwamba ameanza kushughulikia haki mbalimbali za makundi hayo, ambapo kwa sasa wapo kwenye mchakato wa kuishinikiza serikali kusaini mkataba wa kuridhia haki za wasichana wa majumbani.
Aliwapongeza waandishi wa habari kwamba pamoja na changamoto nyingi wanazokutana nazo, lakini hawakati tamaa na wamekuwa wakifanya kazi yao kwa moyo mmoja na kwa bidii.
Kama mkakati wake wa kuwasaidia waandishi wa habari, alisema atasimamia Habari Group ili wawe mabalozi wazuri kwenye mambo mbalimbali kwa jamii, ikiwemo kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali, kuwapa elimu ya umuhimu wa cheti cha kuzaliwa, sambamba na kushirikiana nao bega kwa bega kwenye mambo muhimu ya kijamii.
"Kuwasidia kwenu ni miongoni mwa malengo yangu niliyojiwekea ya kupigania haki ya baadhi ya makundi ambyo nimeona haki zao kama wafanyakazi hazitekelezwi,"aliongeza.
Akizungumza katika hafla hiyo mwanamitindo maarufu nchini Jokate Mwegelo alisema kikundi hicho kitafika mbali endapo watajenga upendo baina yao.
“Haya maisha lazima mjikomboe, na kujikomboa ni kama hivi mnajiunga katika vikundi na mtasonga mbele kinachotakiwa ni kuwa na moyo na kile mnachokifanya…” alisisitiza Jokate.
Alisema kuwa hivi karibuni alianzisha kampuni yake ya kutengeneza nywele na muda si mrefu atasonga mbele kwa kufyatua bidhaa nyingine mpya.
“Tusitegemee wanaume tujenge uwezo wa kusimama sisi kama sisi na tuataendelea, leo hii Beyonce (Mwanamuziki wa Marekani) anaweza kusisimama hata kama akiwa ameachana na Jay Z na hilo ndilo lengo langu, lengo langu ni kukuwa kibiashara zaidi na zaidi nataka kuwa kama Bakhressa” alisisitiza Jokate.

Thursday, April 4, 2013

BALOTELLI ANASEMA MAPENZI YAMEMSAIDIA KUPUNGUZA STRESS

Mario Balotelli Akiwa Na Fanny Robert Neguesh 
Anaitwa Fanny Robert Neguesh Na Kila Anapokwenda Mario Na Yeye Yupo Ni Kama Mapacha Alisema Balotelli


Balotell ambaye wengi humfahamu kwa jina la utani 'mtukutu' amekuwa akionekana mara kwa mara katika sehemu mbalimbali na mpenzi wake huyo na hivi karibuni Balottell alisikika akiwaambia waandishi wa habari kuwa mapenzi ya kweli kutoka kwa kimwana huyo yamemsaidia kupunguza mawazo wakati anahamia AC Millan.

from Sam Misago blogs