Monday, November 30, 2015

Marehemu Mawazo alivyoagwa na wana-CHADEMA Mwanza leo.. (Picha) #RIP


Taarifa iliyotolewa jana na viongozi wa CHADEMA Mwanza ilielekeza utaratibu wa siku tatu mfululizo mpaka mazishi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Geita, Marehemu Alphonce Mawazo.
Leo kuanzia asubuhi taratibu zilianza kwa kuutoa mwili wa Marehemu Hospitali, wakaelekea viwanja vya Furahisha vilivyopo katikati ya Mwanza kwa ajili ya shughuli za kumuaga marehemu ambapo viongozi mbalimbali wa CHADEMA wamewaongoza wanaCHADEMA waliokusanyika katika viwanja hivyo kumuaga marehemu.
Hapa ninazo picha za tukio lote.
index IX
Mzee Edward Lowassa
index VI
Mbunge wa Jimbo la Hai, Freeman Mbowe
index X
Mzee Frederick Sumaye
index XI
Salum Mwalimu
index XXXX
Mtoto wa marehemu Mawazo.
index III index VIII index VVXX index XII index XIII index XV index XX index XXI index XXIII index XXIV index XXV index XXVV index XXXXVV index XXXXXCC index

Friday, November 27, 2015

Wasifu wa Papa Francis na unyenyekevu wake

Papa Francis hupenda sana kutangamana na watu wa kawaida
Papa Francis
Papa Francis ndiye kiongozi wa kwanza wa Kanisa katoliki kutoka mataifa ya Amerika.
Kiongozi huyu alizaliwa mjini Buenos Aires, Argentina 17 Desemba mwaka 1936 na kupewa jina Jorge Mario Bergoglio. Babake, Mario, alikuwa mhasibu katika shirika la reli nchini humo. Mamake Bi Regina Sivori alikuwa tu mke nyumbani aliyeshughulisha zaidi na kuwalewa watoto wake watano.
Ujanani Papa Francis alipenda sana kandanda na aliwahi kufanya kazi za kawaida kama kuwa mlinzi katika jumba la starehe. Na katika shughuli zake za kidini kuna wakati viongozi wa kisiasa wa Argentina walimtaja kama mpinzani wao kisiasa.
Papa Francis hupenda sana kutangamana na watu wa kawaida
Papa Francis anajiita mtu wa kawaida, msemo wake maarufu na ambao ameutumia mara kadhaa ni kwamba, "watu wangu ni maskini na mimi ni mmoja wao".
Si jambo la kushangaza, hivyo basi, kwamba kiongozi huyo ya Wakatoliki bilioni 1. 4 anaishi maisha ya kawaida sana na katika nyumba ya kawaida makao makuu Vatican. Huwa anajipikia mwenyewe chakula chake.
Papa Francis hata kabla ya kuwatazwa kwake na kuwa kiongozi ya Wakatoliki duniani, katika huduma zake za kidini alionekana kama mtu wa kawaida sana, mpenda maskini na watu wa kawaida na asiyetaka makuu.
Hata mavazi yake ya kidini sio yale yaliyo na mapambo mengi.
Hii ni kutokana na kwamba yeye ni wa huduma ya Wa-Jesuit. Wafuasi wa huduma hii ni makasisi waliojitilea kuishi maisha ya umaskini na kuwahudumia zaidi maskini na wasiojiweza miongoni mwa jamii.
Kabla ya kuingilia shughuli za kidini na hatimaye kujiunga na chuo cha mafunzo ya kidini, kiongozi huyo aliwahi kufanya kazi katika maabara na pia kama mlinzi katika jumba moja la starehe huko Argentina. Na baadaye akiwa na umri wa miaka 33 alitawazwa kuwa kasisi wa Kanisa Katoliki
Papa Francis alipokutana na kiongozi wa zamani wa Fidel Castro
Hatimaye alipanda na kuwa Askofu wa jimbo la Buenos Aires mwaka 1998 na miaka miatatu baadaye Papa John Paul II alimtawaza kuwa Kadinali.
Alipokuwa Kadinali serikali za Rais Néstor Kirchner na mrithi wake Cristina Fernández de Kirchner zilimuona kiongozi huo wa kidini kama mpinzani wao kisiasa. Tangu enzi hizo hadi wa leo Papa Francis msimamo wake ni kwamba "Ukimfuata Kristo lazima ufahamu kuwa kuwanyanyasa watu au kuwanyima haki zao ni dhambi kubwa sana.”
Viongozi kadhaa wa dini na madhehebu mengine wamemtaja Papa Francis kama kiongozi mwenye kupenda uhusiano bora miongoni mwa dini na madhehebu tofauti. Kwa mfano mwezi Novemba mwaka 2012 katika Kanisa kuu la Kikatoliki mjini Buenos Aires, Papa Francis aliwaleta pamoja viongozi wa Kiyahudi, Waislamu na madhehebu ya kiinjilisti katika ibada maalum ya pamoja ya kuombea amani na suluhu ya machafuko Mashariki ya Kati.
Papa
Papa Francis na mtangulizi wake Papa Benedict XVI
Na ndio pengine tarehe 13 Machi, 2013 alipochaguliwa kuwa kiongozi wa Wakatoliki wote duniani viongozi wa Kiislamu mjini Buenos Aires walisifu uteuzi wake na kumtaja kama " rafiki wa Waislamu na mtu anayependa kushauriana na watu wa dini zote".

chanzo BBC

Ziara ya Papa Francis!! Hivi ndivyo Wakenya walivyomkaribisha ....

Papa Francis wa kanisa katoliki duniani ameanza ziara yake katika nchi za Afrika na leo alikuwa Kenya.
Papa Francis alilakiwa na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta katika uwanja wa ndege uliopo Nairobi na kuwashukuru Wakenya kwa kumkaribisha vizuri huku akiwatakiwa baraka tele za Mwenyezi Mungu.
Nchi nyingine za Afrika ambazo Papa Francis atatembelea ni pamoja na Uganda pamoja na Jamuhuri ya Afrika ya Kati.
12310702_1176227699072448_7023449470200743242_n

PAPA1
12246753_1176164512412100_9085184381190009282_n

12246609_1176196492408902_5396629347335874284_n
12310605_1176169872411564_3224816055986889371_n

12310524_1176195942408957_6907347762988498579_n

12308666_1176212932407258_4697046452725321664_n
12308425_1176225639072654_7020017918906803636_n

12301729_1176199365741948_6806569745452632934_n
11231854_1176197315742153_8267972046142576520_n

12301629_1176169602411591_6230778873137926893_n

12295369_1176227685739116_4124924506738780839_n

12289727_1176225469072671_9160892973371525038_n

12289632_1176195512409000_8323891445956403269_n

12279179_1176169622411589_8802266997962118971_n

12294743_1176223492406202_249316813490834097_n

PAPA6
PAPA7
a ya kuagwa na maziko ya marehemu Alphonce Mawazo wa Chadema hii hapa, Lowassa, Sumaye na Mbowe kuongoza maombolezo Ratiba ya shughuli ya utoaji heshima za mwisho na mazishi ya Kamanda Mawazo Leo Siku ya Ijumaa, Novemba 27 saa 2 asubuhi, mwili wa Mpiganaji na Kiongozi wetu Alphonce Mawazo utachukuliwa Hospitali ya Bugando kuelekea nyumbani kwa Baba yake mdogo, eneo la Nyegezi-Swea kwa ajili heshima za familia kabla ya kuelekea Viwanja vya Furahisha ambapo Viongozi waandamizi wa UKAWA, wakiongozwa wa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe, Mgombea Urais Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye, wabunge wa UKAWA, wataongoza maelfu ya wakazi wa Jiji la Mwanza na vitongoji vyake kutoa heshima za mwisho kwa mpendwa wao Mawazo. Baada ya Viwanja vya Furahisha, mwili wa Mpiganaji Mawazo utasafirishwa kuelekea Geita kwa ajili ya kuwapatia nafasi wakazi wa Mkoa wa Geita kumuaga Kiongozi wao siku ya Jumamosi, Novemba 28 kuanzia asubuhi mapema ambapo baadae mchana mwili huo utapelekwa Mji Mdogo wa Katoro, mkoani Geita, ambapo pia wananchi watapata fursa ya kumpatia heshima za mwisho na kumuaga Mawazo ambaye alikuwa ni Mgombea wao wa Ubunge wa Jimbo la Busanda. Baada ya wakazi wa Katoro kushiriki tukio hilo, mwili wa Kamanda Mawazo utapelekwa nyumbani kwao kijijini Chikobe tayari kumhifadhi kwenye nyumba ya milele shambani kwake, siku a Jumapili, Novemba 29, baada ya familia, ndugu, jamaa na wakazi wa kijiji hicho kutoa heshima zao za mwisho. Tumaini Makene Msemaji Mkuu Chadema Copy the BEST Traders and Make Money : http://bit.ly/fxzulu

Copy the BEST Traders and Make Money : http://bit.ly/fxzulu

Sentensi 7 za Mbowe nje ya Mahakama baada ya kuruhusiwa kuaga mwili wa marehemu Mawazo Mwanza.

Ishu ya viongozi na wanachama wa CHADEMA kuzuiwa kuaga mwili wa Marehemu Alphonce Mawazo, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Geita imekuwa ikiripotiwa na kuandikwa kwenye vyombo vya habari huku ikisubiriwa kutolewa majibu na Mahakama Kuu Mwanza kuhusu hatma ya zuio hilo.
Leo maamuzi ya Mahakama Kuu Mwanza yametoka na majibu kwamba wanaCHADEMA na viongozi wao wamepata kibali cha Mahakama hiyo kuendelea na shughuli za kuaga pamoja na mazishi ya kiongozi huyo.
Marehemu Alphoince Mawazo kwenye Jukwaa la Kampeni enzi za uhai wake.
Marehemu Alphonce Mawazo kwenye Jukwaa la Kampeni enzi za uhai wake.
Nje ya Mahakama Kuu Mwanza, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Aikael Mbowe alipata dakika chache kuongea na wanachama wa CHADEMA ambao walikuwa wakisubiri kusikia maamuzi ya Mahakama >>>> “Ni lazima tukae vikao kupanga ratiba ya kumuaga Kamanda Mawazo, Jaji ametoa maelekezo kwamba viongozi wa CHADEMA, familia ya marehemu na Jeshi la Polisi wakae pamoja kupanga ratiba kamili.”
index-II3
Tutaheshimu maelekezo ya Jaji lakini hatutakubali kuonewa, muwe na imani kwamba haki itatendeka… tunakwenda kwenye vikao lakini tunahitaji kumaliza jambo hili kuanzia kesho, tutamuaga Mawazo kwa heshima anayostahili katika eneo ambalo tutawatangazia.” >>> Freeman Mbowe.
CDM
Ezekiel Wenje na Salum Mwalimu wakiwa ndani ya Mahakama Mwanza.
index VI
index III
Watu wa usalama nje ya Mahakama Kuu Mwanza.
index IV
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wanaCHADEMA
index V
index
Wakili wa CHADEMA, John Mallya.

Kwa hisani ya Millart Ayo.com
Ratiba ya kuagwa na maziko ya marehemu Alphonce Mawazo wa Chadema hii hapa, Lowassa, Sumaye na Mbowe kuongoza maombolezo Ratiba ya shughuli ya utoaji heshima za mwisho na mazishi ya Kamanda Mawazo Leo Siku ya Ijumaa, Novemba 27 saa 2 asubuhi, mwili wa Mpiganaji na Kiongozi wetu Alphonce Mawazo utachukuliwa Hospitali ya Bugando kuelekea nyumbani kwa Baba yake mdogo, eneo la Nyegezi-Swea kwa ajili heshima za familia kabla ya kuelekea Viwanja vya Furahisha ambapo Viongozi waandamizi wa UKAWA, wakiongozwa wa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe, Mgombea Urais Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye, wabunge wa UKAWA, wataongoza maelfu ya wakazi wa Jiji la Mwanza na vitongoji vyake kutoa heshima za mwisho kwa mpendwa wao Mawazo. Baada ya Viwanja vya Furahisha, mwili wa Mpiganaji Mawazo utasafirishwa kuelekea Geita kwa ajili ya kuwapatia nafasi wakazi wa Mkoa wa Geita kumuaga Kiongozi wao siku ya Jumamosi, Novemba 28 kuanzia asubuhi mapema ambapo baadae mchana mwili huo utapelekwa Mji Mdogo wa Katoro, mkoani Geita, ambapo pia wananchi watapata fursa ya kumpatia heshima za mwisho na kumuaga Mawazo ambaye alikuwa ni Mgombea wao wa Ubunge wa Jimbo la Busanda. Baada ya wakazi wa Katoro kushiriki tukio hilo, mwili wa Kamanda Mawazo utapelekwa nyumbani kwao kijijini Chikobe tayari kumhifadhi kwenye nyumba ya milele shambani kwake, siku a Jumapili, Novemba 29, baada ya familia, ndugu, jamaa na wakazi wa kijiji hicho kutoa heshima zao za mwisho. Tumaini Makene Copy the BEST Traders and Make Money : http://bit.ly/fxzulu

Copy the BEST Traders and Make Money : http://bit.ly/fxzulu