Wednesday, May 8, 2013

Soma tamko lote la Ruge Mutahaba dhidi ya Lady Jay Dee

KATIKA siku za hivi karibuni katika vyombo vya habari hasa hasa kwenye mitandao ya kijamii nchini kumekuwa na taarifa rasmi na zisizo rasmi kutoka kwa Mwanamuziki Lady Jaydee alilalamikia Kituo chetu cha Clouds FM na wakurugenzi wake Ruge Mutahaba na Joseph Kussaga.
Ruge Mutahaba akizungumzia mustakabali wa Made in Tanzania sambamba na sakata lao na Lady Jay Dee
Kwa mtazamo wangu, kila mwananchi ana haki ya kutoa maoni yake ingawa kwenye nchi yetu ya Tanzania, tumezoea maoni hayo kutolewa kwa lugha ya ustaraabu na staha.
Maoni kuhusu nani wa kuja kwenye msiba wako au nyimbo za kupigwa kwenye msiba wako ni haki ya kila mwananchi na hakuna atayeuingilia uamuzi huo. Maoni pia ya redio gani mtu anaipenda au tv gani pia nayo ni utashi wa mtu mwenyewe.

No comments:

Post a Comment