Sunday, April 19, 2015

WATANZANIA tusimame kupinga mauaji ya albino - Lowassa

WATANZANIA wametakiwa kulaani na kukemea mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi albino kwa kuwa matukio hayo yanaitia aibu nchi ya Tanzania na kupoteza sifa yake, kuwa nchi yenye amani.

Aidha Chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi Tanzania (TAS) kimetakiwa kushawishi majina ya watu 16 waliohukumiwa kifo kutokana na mauaji ya watu wenye ualbino kumfikia mapema Rais Jakaya Kikwete ili kutoa hakumu.

Wito huo ulitolewa Jijini Dar es salaam jana na Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa wakati akihutubia mamia ya vijana walioshiriki katika matembezi ya hiyari ya kulaani na kupinga mauaji, ukataji wa viungo pamoja na ufukuaji wa makaburi ya watu wenye ualbino.

Lowassa akiwa mwenye afya njema akiwa na wabunge, madiwani pamoja na watu wenye ulemavu huo walitembea umbali wa kilometa tano kuanzia Uwanja wa Taifa na kupitia Temeke Hospitali, Chang'ombe Polisi, Shule ya Sek
ondari Kibasila na kumalizia katika viwanja vya TCC Club kwa kutumia dakika 25.

REGINALD MENGI AHOFIA KUULIWA NA SERIKALI YA KIKWETE,SOMA HAPA KUJUA::


Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi amesema anahofia usalama  wa maisha yake, kufuatia habari iliyoandikwa katika gazeti moja la kila wiki  kwamba,  Rais Jakaya Kikwete aliapa kupambana naye jambo ambalo limempa hofu kubwa.
         Kadhalika, amelalamikia  Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu na Idara ya Habari Maelezo kwa kukaa kimya na kuacha kutoa ufafanuzi dhidi ya tuhuma hizo, huku taarifa hizo zikiendelea kusambazwa.
         Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mengi alisema kuwa tuhuma zilizotolewa dhidi yake kuwa yeye ni kinara wa kuhujumu serikali ya Rais Kikwete siyo za kweli.
         Dk.Mengi alisema amesoma kwa masikitiko makubwa habari iliyochapishwa Machi 23, mwaka huu na gazeti la Taifa Imara, yenye kichwa cha habari 'Zitto amchongea Mengi kwa JK' ambapo pamoja na mambo mengine inasema kuwa Zitto Kabwe amemchongea Dk. Mengi kwa Rais Kikwete kwamba ndiye kinara wa kuhujumu serikali yake.
          Alisema habari hiyo ambayo chanzo chake kimeelezwa kwamba ni Ikulu, iliendelea kueleza kuwa Zitto alikutana na Rais Kikwete muda mfupi baada ya kuwasilisha bungeni ripoti ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusiana na kashfa ya Escrow ambayo Zitto alikuwa ni mwenyekiti wake.
       "Habari hiyo inasema kwamba katika mazungumzo yake na Rais Kikwete Zitto amenukuliwa akimueleza mkuu huyo wa nchi kuwa anayesababisha serikali yake iyumbe kila mara ni Mengi," alisema Dk. Mengi.
      Dk. Mengi alisema habari hiyo ambayo nakala yake ameiambatanisha kwenye taarifa yake, inasema yeye Zitto , binafsi amekuwa akishawishiwa na Dk. Mengi kuiangusha serikali ya Rais Kikwete.
     Hata hivyo, Dk. Mengi alisema katika habari hiyo Zitto alikwenda mbali zaidi kumueleza Rais Kikwete kuwa Dk. Mengi ameapa kuwa Rais Kikwete akimaliza muda wake wa Urais atamshughulikia kwa nguvu zake zote.
     Alisema habari hiyo imeeleza kwamba baada ya maelezo hayo, Rais Kikwete aliapa kupambana na Dk. Mengi na akamshukuru Zitto kwa kumpa taarifa hizo.
    Mengi alisema tuhuma zilizotolewa kuhusu nia yake ya kutaka kuiangusha serikali ya Rais Kikwete na kumshughulikia baada ya kumaliza muda wake wa uongozi, zimemshtua sana na tamko la kwamba Rais Kikwete aliapa kuwa atapambana na yeye zimempa hofu kuhusu mustakabali wa maisha yake.
     Alisema kuwa hofu yake kubwa inasababishwa na Ikulu na Idara ya habari Maelezo kukaa kimya kwa zaidi ya wiki tatu bila kutoa ufafanuzi wowote.
    "Najua umakini wa Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu na Idara ya habari Maelezo katika kutoa ufafanuzi wa haraka wa jambo lolote linalomhusu Rais, lakini katika hili nashangaa kuona taasisi hizo zimeamua kukaa kimya na kuacha tuhuma hizo kusambaa,"alisema Dk. Mengi.
    Aliongezea kusema kuwa," hofu yangu inazidi kuwa kubwa kwa sababu Rais ni Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama. Kauli yake kama ilivyonukuliwa na gazeti hili kwamba atapambana na mimi inawezekana kuchukuliwa kama agizo kwa vyombo vya dola kuniangamiza," alisema.
         Alitolea mfano mwaka 1170, Askofu Mkuu wa Canterbury nchini Uingereza aliuawa baada ya walinzi wa mfalme kusikia mfalme akisema "hakuna anayeweza kuniondolea huyo mkorofi?". Walinzi wake wakadhani mfalme ameagiza wamuue Askofu huyo na wakamuua, alisema.

CHANZO: NIPASHE

WAHARIRIR WAIGOMEA SHERIA YA MTANDAONI





Ni kama wamegoma, Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini wameitaka serikali kuacha kuharakisha zoezi la kutia saini sheria ya mtandaoni badala yake wajikite kutoa Elimu kwa watanzania ili sheria hiyo ifahamike,
Wakizungumza katika Mkutano maalum ulioitishwa na wizara ukilenga kuwapa elimu juu ya sheria hiyo inayosubiri kuwekwa saini na Mh. Rais Jakaya Kiwete, wamesema sheria hiyo inamatatizo na inahitaji muda wadau waipitie na kuielewa,

Wamesema makosa yaliyoainishwa katika sheria hiyo ambao kama ikitiwa saini na kuanza kutumika, inaweza kuwabana watu ambao hawahusiki.
Baadhi ya makosa yaliyoanishwa katika sheria hiyo ni pamoja na kutuma taarifa bila ridhaa ya mtu, kusambaza picha za ngono na za utupu, udanganyifu unaohusiana na kompyuta, makosa yanayohusiana na utambuzi, kughushi kunakohusiana na masuala ya kompyuta na kusambaza picha za utupu za watoto.
Mengine ni unyanyasaji kwa kutumia mtandao, kuchapisha taarifa yoyote ambayo itasababisha mauaji ya kimbari, uongo na matusi ya kibaguzi, huku adhabu kali ikiwa ni faini ya Sh50 milioni au kifungo kisichopungua  miaka saba, kwa mtu atakayebainika kusambaza picha za ngono mtandaoni.
Sheria hiyo pia iliwahi pia kulalamikiwa na Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika aliyeitaka Serikali ikusanye maoni ya wadau kabla ya kuwasilisha muswada huo kwa hati ya dharua kutokana na umuhimu wake kwa jamii.
Wamedai kuwa sheria hiyo inaweza kuifanya Tanzania ikawa ni kati ya nchi adui wa matumizi ya mtandao wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama).
“Sheria hii itamuathiri mtu yeyote anayeweza kutumia mtandao wa intaneti kwa kutumia kifaa chochote iwe kompyuta kubwa au vifaa vyenye uwezo wa kufanya kazi kama kompyuta kama simu za kiganjani, televisheni na vifaa vingine vinavyoendana na hivyo,”Amesema Peter Nyanje Mhariri wa the Citizen.

TAIFA LIMETIKISIKA NA AJALI YA MBAYA MKOANI MBEYA,TIZAMA HAPA


Ajali ya Daladala imeua watu 19 eneo maarufu kama Uwanja wa ndege, Kiwila, Mkoani Mbeya baada ya daladala hiyo kutumbukia kwenye Mto.
 
Habari  toka  eneo la tukio zinaarifu kuwa watu wawili tu ndio wamepona akiwemo kondakta. 
 
Ajali hii imetokea baada  ya Coaster zinazofanya safari zake kati ya Mbeya na Kyela kugoma hivyo baadhi ya daladala za mjini kuamua kubeba abiria.




 SOURCE Mpekuzi blog