Ibada maalum ya kumuombea Padre
Evarist Mushi imefanyika leo Zanzibar kwenye kanisa katoliki la St.
Joseph la Minara miwili na kuongozwa na Askofu mkuu Muadhama Polycarp
Cardinal Pengo na kuhudhuriwa na mamia ya waumini wa kanisa hilo.
Wengine waliohudhuria ni
viongozi mbalimbali wa kiserikali wakiongozwa na Rais wa Zanzibar na
mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohamed Shein ambapo baada ya
ibada safari ya kuelekea Kitope kwenye maziko ilianza kwa msafara wa
magari mengi kupita mitaani huku ukiongozwa na gari la Polisi.
Padri Evarist Mushi wa Kanisa
katoliki la St Joseph la Minara Miwili aliuwawa kwa kupigwa risasi na
watu wasiojulikana wakati akielekea kwenye ibada ya jumapili ya Kanisa
la St. Theresia lililoko Mtoni.
by millard ayo.com
No comments:
Post a Comment