Wednesday, February 20, 2013

PICHA ZA KWENYE IBADA YA MWISHO YA PADRI MUSHI

Kanisa la St. Joseph Minara miwili.
.
.
.
Ibada maalum ya kumuombea Padre Evarist Mushi imefanyika leo Zanzibar kwenye kanisa katoliki la St. Joseph la Minara miwili na kuongozwa na Askofu mkuu Muadhama Polycarp Cardinal Pengo na kuhudhuriwa na mamia ya waumini wa kanisa hilo.
Wengine waliohudhuria ni viongozi mbalimbali wa kiserikali wakiongozwa na Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohamed Shein ambapo baada ya ibada safari ya kuelekea Kitope kwenye maziko ilianza kwa msafara wa magari mengi kupita mitaani huku ukiongozwa na gari la Polisi.
Padri Evarist Mushi wa Kanisa katoliki la St Joseph la Minara Miwili aliuwawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana wakati akielekea kwenye ibada ya jumapili ya Kanisa la St. Theresia lililoko Mtoni.

by millard ayo.com

Tuesday, February 19, 2013

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE HAYA HAPA






















Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa (MB) leo ametangaza rasmi matokeo ya Mitihani ya Kidato cha Nne, maarifa-QT.
---------------
TAARIFA YA MATOKEO YA MITIHANI YA MAARIFA (QT) NA KIDATO CHA NNE (CSEE)
ILIYOFANYIKA OKTOBA 2012
---------------------
1.0                 UTANGULIZI
Mitihani ya Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT) kwa mwaka 2012 ilifanyika nchini kote kuanzia tarehe 8-25 Oktoba 2012.  Napenda kuchukua nafasi hii kutangaza rasmi matokeo ya mitihani hiyo kama ifuatavyo :
2.0                 MTIHANI WA MAARIFA (QT)
2.1           Usajili na Mahudhurio
Katika Mtihani wa Maarifa 2012 watahiniwa waliosajiliwa ni 21,310 ambapo wasichana walikuwa ni 13,134 na wavulana ni 8,176
Jumla ya watahiniwa 17,137 sawa na asilimia 80.42 ya waliosajiliwa wamefanya Mtihani. 
2.2          Matokeo ya Mtihani wa Maarifa (QT)
Watahiniwa 5,984 kati ya 17,137 waliofanya mtihani wamefaulu Mtihani wa Maarifa (QT).
3.0                 MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2012
Jumla ya vituo 5,058 vilitumika katika kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 ambapo vituo 4,155 vilikuwa vya watahiniwa wa shule na vituo 903 vilikuwa ni vya watahiniwa wa kujitegemea.
3.1                 Usajili na Mahudhurio ya Watahiniwa
(a)           Watahiniwa Wote
Jumla ya watahiniwa 480,036 walisajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 wakiwemo wasichana 217,583 sawa na asilimia 45.33 na wavulana 262,453 sawa na asilimia 54.67.  Watahiniwa waliofanya mtihani wa Kidato cha Nne 2012  ni 456,137 sawa na asilimia 95.44. Watahiniwa 21,820 sawa na asilimia 4.55 ya watahiniwa wote waliosajiliwa hawakufanya mtihani.
(b)            Watahiniwa wa Shule
Watahiniwa wa shule waliosajiliwa ni 411,230 wakiwemo wasichana 182,978 sawa na asilimia 44.50 na wavulana 228,252 sawa na asilimia 55.50.  Watahiniwa wa shule waliofanya mtihani walikuwa 397,136 sawa na asilimia 96.57. Aidha, watahiniwa 14,090 sawa na asilimia 3.43 hawakufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo utoro,  ugonjwa na vifo.
(c)             Watahiniwa wa Kujitegemea
Watahiniwa wa kujitegemea waliosajiliwa walikuwa ni 68,806 wakiwemo wasichana 34,605 sawa na asilimia 50.29 na wavulana 34,201 sawa na asilimia 49.71. Watahiniwa 61,001 wakiwemo wasichana 30,917 na wavulana 30,084  wamefanya mtihani wakati watahiniwa 7,730 sawa na asilimia 11.23  hawakufanya mtihani.
4.0                 MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE
(a)                 Watahiniwa wa Shule
Jumla ya watahiniwa wa shule 126,847 kati ya watahiniwa 397,136 waliofanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 wamefaulu. Wasichana waliofaulu ni 46,161 na wavulana ni 80,686.
(b)                Watahiniwa wa Kujitegemea
Idadi ya watahiniwa wa kujitegemea waliofaulu mtihani ni 16,112 kati ya watahiniwa 61,001 waliofanya mtihani.  Wasichana waliofaulu ni 6,751 na wavulana ni 9,361. 
5.0                 UBORA WA UFAULU KWA MADARAJA NA JINSI
Ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa wa shule unaonesha kuwa jumla ya watahiniwa 23,520 wamefaulu katika madaraja I – III ambapo kati yao wasichana ni 7,178 na wavulana ni 16,342.
Mchanganuo wa ufaulu kwa kila Daraja kwa jinsi kwa Watahiniwa wa Shule mwaka 2012 ni kama ifuatavyo:
Idadi ya Wavulana      
Idadi ya  Wasichana
Jumla
I
1,073
568
1,641
II
4,456
1,997
6,453
III
10,813
4,613
15,426
I-III
16,342
7,178
23,520
IV
64,344
38,983
103,327
0
120,664
120,239
240,903
6.0        SHULE ISHIRINI ZILIZOFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA KUNDI LA SHULE ZENYE WATAHINIWA 40 AU ZAIDI
------------
Ubora wa ufaulu wa shule umepangwa kwa kutumia kigezo cha “Grade Point Average” (GPA) kuanzia A = 1 hadi F = 5.  Shule zenye watahiniwa 40 na zaidi ziko 3,391. Shule ya kwanza hadi ya ishirini zimeainishwa kwenye Jedwali lifuatalo :
NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI YA WATAHINIWA
MKOA
1
ST. FRANCIS GIRLS
90
MBEYA
2
MARIAN BOYS S.S
75
PWANI
3
FEZA BOYS S.S
69
DAR ES SALAAM
4
MARIAN GIRLS S.S
88
PWANI
5
ROSMINI  S S
78
TANGA
6
CANOSSA S.S
66
DAR ES SALAAM
7
JUDE MOSHONO S S
51
ARUSHA
8
ST. MARY’S  MAZINDE JUU
83
TANGA
9
ANWARITE GIRLS S S
49
KILIMANJARO
10
KIFUNGILO  GIRLS S S
86
TANGA
11
FEZA GIRLS
49
DAR ES SALAAM
12
KANDOTO SAYANSI GIRLS SS
124
KILIMANJARO
13
DON BOSCO SEMINARY SS
43
IRINGA
14
ST.JOSEPH MILLENIUM
133
DAR ES SALAAM
15
ST.JOSEPH’S ITERAMBOGO SS
64
KIGOMA
16
ST.JAMES SEMINARY SS
44
KILIMANJARO
17
MZUMBE SS
104
MOROGORO
18
KIBAHA SS
108
PWANI
19
NYEGEZI SEMINARY SS
68
MWANZA
20
TENGERU BOYS SS
76
ARUSHA
7.0        SHULE KUMI AMBAZO HAZIKUFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA KUNDI LA SHULE ZENYE WATAHINIWA 40 AU ZAIDI
NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI YA WATAHINIWA
MKOA
1
MIBUYUNI S.S
40
 LINDI
2
NDAME  S.S
41
UNGUJA
3
MAMNDIMKONGO S.S
63
PWANI
4
CHITEKETE S.S
57
MTWARA
5
MAENDELEO S.S
103
DAR ES SALAAM
6
KWAMNDOLWA S.S
89
TANGA
7
UNGULU S.S
62
MOROGORO
8
KIKALE S.S
60
PWANI
9
NKUMBA S.S
152
TANGA
10
TONGONI S.S
56
TANGA
8.0           TATHMINI YA UFAULU WA WATAHINIWA WA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE MWAKA 2012 
8.1           Tathmini ya awali iliyofanyika kuhusu ufaulu wa watahiniwa katika shule mbalimbali inaonesha kuwa shule zilizofanya vizuri zaidi ni zile ambazo zina mahitaji yote ya msingi ikiwemo walimu wa kutosha, miundombinu na vifaa vya kufundishia na kujifunzia.  Aidha, shule zenye ufaulu wa chini ni zile ambazo zina changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na:
(i)         Baadhi ya shule za vijijini hazina kabisa walimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati na pia zina upungufu mkubwa wa walimu wa masomo mengine;
(ii)        Kutokuwepo kwa maabara kwa shule zenye mikondo ya sayansi na pia kutokuwepo kwa maktaba kwa ajili ya kujisomea; na
(iii)       Upungufu mkubwa wa vitabu vya kiada na ziada. Katika baadhi ya shule uwiano wa kitabu kwa mwanafunzi ni 1:10.
8.2           Mkakati wa Serikali ni kuendelea kupunguza changamoto hizo kila mwaka ikiwa ni pamoja na kufanya mambo yafuatayo:
(i)             Kuajiri walimu kila mwaka ili kuondoa upungufu uliopo katika shule zetu. Mwaka 2011/2012 Serikali iliajiri walimu wa sekodari 13,246 na mwaka huu wa fedha 2012/2013 imeajiri walimu 12,973 ambao wamepangwa katika shule zenye upungufu mkubwa wa walimu. Ajira ya walimu wapya mwaka huu umetuwezesha kuwa na wastani wa walimu 2-3 kwa shule.  Hali hii itaendelea kuboreka kadri tunavyoendela kuajiri walimu.
(ii)            Kuboresha miundombinu iliyoko katika shule zetu ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba za walimu, madarasa na maabara. Mwaka 2012/2013 Serikali imepanga kuboresha miundombinu katika shule 264 zilizopo katika mazingira magumu ikiwemo miundombinu ya maabara na nyumba za walimu.
(iii)           Kuendelea kutoa ruzuku ya Tsh 25,000 kwa mwanafunzi kwa mwaka, ambapo asilimia 50 ya fedha hizo ni kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia ili kuziwezesha shule kununua vitabu pamoja na vifaa vingine muhimu kitaaluma.
(iv)           Wizara kuendelea kuzishauri Halmashauri kuweka mgawanyo mzuri wa walimu waliopo baina ya shule na shule.
(v)            Wizara itaendelea kuimarisha Idara ya Ukaguzi wa Shule pamoja na kuwawezesha Waratibu Elimu Kata na Wakuu wa Shule kufanya ukaguzi wa ndani katika Shule za Sekondari zilizo katika maeneo yao.
9.0           MATOKEO YA MITIHANI YALIYOZUIWA
Baraza la Mitihani la Tanzania limezuia kutoa matokeo ya:
(a)           Watahiniwa 28,582 wa Shule ambao hawajalipa ada ya Mtihani hadi watakapolipa ada wanayodaiwa pamoja na faini; na ikiwa hawatalipa katika kipindi cha miaka miwili (02) toka matokeo kutangazwa, matokeo yao yatafutwa.
(b)           Watahiniwa 65 wa kujitegemea na 71 waliofanya Mtihani wa Maarifa (QT) mwaka 2012 bila ya kulipa ada ya Mtihani hadi watakapolipa ada pamoja na faini. Ikiwa hawatalipa ada hiyo katika kipindi cha miaka miwili (02) toka matokeo kutangazwa, matokeo yao yatafutwa.
10.0        MATOKEO YA MITIHANI  YALIYOFUTWA
10.1              Matokeo Yaliyofutwa Kwa Sababu ya Udanganyifu
Jumla ya watahiniwa 789 wamefutiwa matokeo yao yote ya mtihani kwa mujibu wa kifungu Na.52(b) cha Kanuni za Mitihani baada ya kubainika kuwa walifanya udanganyifu katika mitihani ya Oktoba 2012. Kati yao, watahiniwa wa shule ni 624 na watahiniwa wa kujitegema ni 148 na watahiniwa wa Mtihani wa Maarifa (QT) ni 17.
Aina ya udanganyifu uliobainika na idadi ya watahiniwa husika ni kama ifuatavyo:
S/N
AINA YA UDANGANYIFU
IDADI YA WATAHINIWA
(i)        
Watahiniwa kubainika kuwa na skripti zenye miandiko tofauti au kuwa na miandiko tofauti katika skripti ya somo moja au zaidi ya moja.
04
(ii)       
Watahiniwa kukamatwa na wasimamizi ndani ya chumba cha mtihani wakiwa na ‘notes.’
170
(iii)      
Watahiniwa kubainika kuwa na mfanano usio wa kawaida wa majibu.
590
(iv)      
Watu kukamatwa wakiwafanyia watahiniwa wengine mtihani ‘impersonation”.
04
(v)       
Watahiniwa kukamatwa na simu ndani ya chumba cha mtihani.
06
(vi)      
Watahiniwa kukamatwa na wasimamizi wakibadilisha karatasi za maswali au skripti kwa lengo la kufanya udanganyifu.
15

JUMLA
789
10.2              Matokeo Yaliyofutwa Kwa Sababu ya Watahiniwa Kuandika Matusi Katika Skripti Zao
-----------
(i)          Jumla ya watahiniwa 24 waliandika matusi kwenye skripti zao za masomo mbalimbali. Kitendo hicho ni kosa kwa mujibu wa kifungu 5(13) cha Kanuni za Mitihani kinachosomeka:
“Written responses to any examination question which carry words, drawings or pictures connected to sex or abusive language in such a way that it becomes offensive shall consitute an examination offence and a candidate who commits such an offence shall be punished by the Council.”
Kutokana na kosa hilo Baraza la Mitihani limefuta matokeo  yao yote kwa mujibu wa Kifungu cha 6(2)(a) cha Kanuni za Mitihani kinachosomeka:  
“A candidate found to have committed an examination offence shall – (a) have his examination results nullified”
(ii)         Kitendo cha kuandika matusi kwenye karatasi za majibu (skripti) kinaonesha utovu wa nidhamu wa hali ya juu. Serikali haitaweza kuwavumilia hata kidogo watahiniwa wa aina hiyo. Hivyo, Serikali itaangalia hatua zaidi za kisheria za kuchukua dhidi ya watahiniwa wote walioandika matusi.
Kwa mujibu wa kifungu Na. 6(2)(b) cha Kanuni za Mitihani, watahiniwa wote waliobainika kufanya udanganyifu katika mitihani au kuandika matusi katika skripti zao hawataruhusiwa kufanya mitihani inayoendeshwa na Baraza la Mitihani la Tanzania  kwa kipindi cha mwaka mmoja (01) kuanzia tarehe ya kutangazwa kwa matokeo.
11.0        KUANGALIA MATOKEO YA MTIHANI WA CSEE na QT, 2012
(a)           Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT), 2012  yanapatikana katika tovuti zifuatazo: 
·               www.matokeo.necta.go.tz,
·               www.necta.go.tz,     
·               www.udsm.edu.ac.tz, au
·               http://www.moe.go.tz
(b)           Matokeo yanaweza kupatikana pia kwa njia ya  ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kwenda namba 15311. Jinsi ya kutuma ujumbe andika:
MATOKEOXNAMBA YA KITUOXNAMBA YA MTAHINIWA
(Mfano : matokeoxS0101x0503)

Dkt.  Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb)

WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

18 Februari 2013

PADRI MUSHI KUZIKWA KESHO....

PADRI Evarist Mushi (55), aliyeuawa juzi kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana Zanzibar, anatazamiwa kuzikwa Kitope katika eneo lililotengwa la makaburi ya mapadri.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Askofu wa Kanisa Katoliki, Jimbo la Zanzibar, Augostino Shao, alisema maandalizi ya maziko yanaendelea vizuri.

“Tunatarajia kuupumzisha mwili wa marehemu Mushi katika makaburi ya Kitope ambako kuna sehemu maalumu ya kuzikwa mapadri,” alisema.

Marehemu Mushi atakuwa Padri wa tatu kuzikwa eneo hilo mkoani Kaskazini Unguja, ambako alisema kwa sasa ni mapema kujua viongozi watakaohudhuria maziko.

Akielezea jinsi alivyopokea taarifa ya kifo cha Padri Mushi, ambaye alikuwa Msaidizi wake Mkuu, Askofu Shao alisema alipokea wakati akiendesha ibada ya kawaida ya Jumapili katika Kanisa la Minara Miwili.

“Nilikuwa naongoza ibada, lakini wenzangu tayari walikuwa wamepata taarifa ya kifo cha Padri Mushi.

Nilikuwa naye asubuhi saa 12 tukaagana, naye akaenda kuongoza misa Mtoni katika Kanisa la Beit-el-Ras,” alisema.

Askofu Shao alivitaka vyombo vya ulinzi, kufanya kazi za kusaka wahalifu kwani jamii tayari imeanza kupoteza imani.

Padri Mushi aliuawa kwa risasi tatu alizopigwa kichwani na watu wasiojulikana juzi saa moja asubuhi, akienda kanisani kuongoza ibada.

Akiwa katika gari lake aina ya Toyota Hilux Surf, Padri Mushi alipigwa risasi kichwani kupitia dirisha la mlango wa kulia.

Mauaji hayo yalifanyika wakati akikata kona kuingia kanisani, ambako watu hao walikuwa wakimsubiri wakiwa na usafiri wa Vespa na baada ya kumpiga risasi walikimbia.
Kutokana na hali hiyo, gari la Padri Mushi lilipoteza mwelekeo na kupamia ukuta wa nyumba iliyo meta chache kutoka Kanisa la Mtakatifu Theresia, ambako alikuwa akienda.

Monday, February 18, 2013

MAUAJI YA PADRI WA KANISA KATOLIKI KWA KUPIGWA RISASI WAKATI AKIENDA KANISANI ZANZIBAR


Picha tofauti za Padri wa Kanisa Katoliki, Padri Evarist Mushi zikimuonesha enzi za uhai wake, Padri Mushi ambaye ameuawa leo asubuhi kwa kupigwa risasi wakati akiingia Kanisani kwa ajili ya Ibada ya Jumapili katika eneo la Mtoni Mjini Magharibi Zanzibar.  
 Hapa ni katika eneo la tukio la mauaji ya Padri Evarist Mushi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi (wa pili kushoto) akiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mohamed Aboud walipotembelea eneo la tukio leo.
 Gari alilokuwa amepanda Padri Evarist Mushi likiwa limetapakaa damu baada ya kupigwa risasi
Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi akizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar leo kufuatia mauaji ya Padri wea Kanisa katoliki, Padri evarist Mushi. (Picha na Adrew Chale, Zanzibar) kwa hisani ya Bashir Nkoromo.

Friday, February 15, 2013

HOSPITALI IMETHIBITISHA KIFO CHA MSANII GOLDIE HARVEY,YAELEZA KILICHOSABABISHA KIFO HICHO

 Hatimaye Daktari kutoka  hospitali ambayo Goldie Harvey alipelekwa Reddington Hospital huko Nigeria,amethibitisha kutokea kwa kifo cha msanii na aliyewahi kushiriki BBA kuwa ni kweli amefariki dunia huko Nigeria saa 5 usiku jana.Inasemakana kuwa ugonjwa uliosababisha kifo cha Goldie huyo ni 'pulmonary embolism'.
'Pulmonary Embolism' ni  Ugonjwa wa Kuganda kwa Damu ,ambao husababisha mshipa mkubwa unaosafirisha damu na hewa kwenda kwenye mapafu kuziba.Husababisha mtu kufariki ghalfa.

'Mungu ailaze roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi'
  ameen.....

Monday, February 11, 2013

Papa Penedict wa XVI AJIUZULU....



Habari kutoka Vatican leo hii zimethibitisha kuwa Papa Benedict XVI atajiuzulu kutoka katika nafasi yake hiyo Februari 28 mwaka huu kutokana na Umri wake kuwa mkubwa mno na kupelekea kupungua uwezo wa utendaji wa kazi zake.
Father Federico Lombardi ambaye ndiye msemaji wa Papa ametoa taarifa hizi rasmi leo  kwa vyombo vya habari, ikiwa ni ujumbe wa moja kwa moja kutoka kwa Papa kwa makadinali wa kanisa hilo duniani.
Papa huyu atatimiza umri wa miaka 86 tarehe 16 mwezi April na alichaguliwa kushika nafasi hii mwaka 2005 akiwa mjerumani wa 6 kushika nafasi hiyo ya juu katika kanisa Katoliki na wa kwanza kabisa kuhudumia kanisa kama papa kutokea karne ya 21.

 Ufuatao ni waraka wake alioutoa leo kwa vyombo vya habari......

Dear Brothers,
I have convoked you to this Consistory, not only for the three canonisations, but also to communicate to you a decision of great importance for the life of the Church. After having repeatedly examined my conscience before God, I have come to the certainty that my strengths, due to an advanced age, are no longer suited to an adequate exercise of the Petrine ministry.

I am well aware that this ministry, due to its essential spiritual nature, must be carried out not only with words and deeds, but no less with prayer and suffering. However, in today’s world, subject to so many rapid changes and shaken by questions of deep relevance for the life of faith, in order to govern the bark of Saint Peter and proclaim the Gospel, both strength of mind and body are necessary, strength which in the last few months, has deteriorated in me to the extent that I have had to recognise my incapacity to adequately fulfil the ministry entrusted to me.

For this reason, and well aware of the seriousness of this act, with full freedom I declare that I renounce the ministry of Bishop of Rome, Successor of Saint Peter, entrusted to me by the Cardinals on 19 April 2005, in such a way, that as from 28 February 2013, at 20:00 hours, the See of Rome, the See of Saint Peter, will be vacant and a Conclave to elect the new Supreme Pontiff will have to be convoked by those whose competence it is.

Dear Brothers, I thank you most sincerely for all the love and work with which you have supported me in my ministry and I ask pardon for all my defects. And now, let us entrust the Holy Church to the care of Our Supreme Pastor, Our Lord Jesus Christ, and implore his holy Mother Mary, so that she may assist the Cardinal Fathers with her maternal solicitude, in electing a new Supreme Pontiff. With regard to myself, I wish to also devotedly serve the Holy Church of God in the future through a life dedicated to prayer.

From the Vatican, 10 February 2013
BENEDICTUS PP XVI