Friday, June 26, 2015


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhVfoQ_iUIh9e0vLTzfXlw3gU0DwuVY9pXeMeF9RYBbjUCPka283TgFhSRMepv820WcgghRG0dz5YuVFUn1HH8F1Jj8EVljxKn513KhCTSCi0PfYAnka3SRlSkCPH93PdRE_lkv_PD5OSo/s1600/MMGL0703.jpg
 Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, akihutubia wanachama wa CCM na wananchi katika Uwanja wa CCM mkoani Manyara baada ya kupokea orodha ya majina 42,405 waliomdhamini kugombea urais
 Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, akipokea orodha ya majina 42,405 kwa Katibu wa CCM Wilaya Manyara, Daniel Ole Porukwa,  waliomdhamini kugombea urais
 Lowassa akisalimiana na wananchi wa Manyara.
 Msafara huo
 Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (katikati),akifurahia jambo katika Mkutano  wa wanachama cha Mapinduzi (CCM) wakati wa kupokea orodha ya majina 42,405 waliomdhamini kugombea urais leo.
 Msafara wa Lowassa.
 Kada wa CCM Mkoani Manyara, akitembea kwa mikono kuonyesha kuanza safari ya matumani kuanza rasmi,wakati wa kumkabidhi Waziri Mkuu wa zamani,orodha ya majina 42,405 waliomdhamini kugombea urais
 Akipeana mkono na kada huyo.PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
Posted by MROKI On Thursday, June 25, 2015 No comments


Makamu wa Rais wa Burundi, Gervais Rufyikiri ameondoka nchini humo kwa kile alichodai kukimbia kusumbuliwa baada ya kupingana na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi kutaka kuongeza kipindi cha tatu cha kuitawala nchi hiyo.
Rufyikiri ameiambia kituo cha Televisheni cha France24, kuongeza muhula wa tatu kwa Rais itakuwa ni kinyume cha matakwa ya katiba.
Aidha Msemaji wa serikali ya Burundi amekanusha madai hayo na kusema kuwa Rufyikiri, amesafiri nje ya nchi kwa shughuli za kikazi.

Bwana Rufikiri amesema amekimbilia usalama wake akidai kuwa maisha yake yamo hatarini.

Msemaji huyo wa serikali amesema iwapo bwana Rufikiri ametoroka Burundi ni kwa maslahi yake mwenyewe wala hakuna yeyote aliyemtishia maisha yake.
Pia taarifa zinasema kuwa mbali na Makamu huyo wa Rais lakini pia Spika wa Bunge la Burundi, Pie Ntavyohanyuma hayupo nchini humo na inasemekana amekwenda Ubelgiji kwa matibabu.
Spika huyo pia anadaiwa kupingana na hitaji hilo la Rais Nkurunzinza la kugombea tena.
Tangu mwezi Aprili mwaka huu Burundi inakabiliwa na maandamano ya mara kwa mara na watu kufa kutokana uamuzi wa Rais Nkurunzinza kutaka kugombea tena katika uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu.
Posted by MROKI On Thursday, June 25, 2015 No comments
 Mwandishi wa habari Edson Kamukara (pichani) amefariki dunia leo.

Taarifa zilizotufikia zinaarifu kuwa Mwandishi huyo aliyepata kuandikia gazeti la Tanzania Daima na baadae kuhamia Mwanahalisi amefikwa na umauti baada ya kulipukiwa na jiko la gesi nyumbani kwake Mabibo jijini Dar es Salaam.
Aidha habari kutoka kwa majirani zinaarifu kuwa Kamukara amerejea kutoka Bukoba, na alijisikia vibaya wakati anaenda dukani kununua dawa akaanguka na majirani kusaidia kumpepea na baade kupelekwa kwake ambako alipumzika hadi alipopata nguvu na kuamua kujiandalia chakula na ndipo ajali hiyo kumfika na kugharimu maisha yake.

Father Kidevu Blog inatoa pole kwa wote waliofikwa na Msiba huo na italeta taarifa kamili hapo baadae.
 Edson (kushoto) enzi za uhai wake akiwa na waandishi wenzake. Kutoka Kulia Mpigapicha Michael Matemanga, Mary Edward, Abdalla Bawaziri na Kurwa Karedia.
Edson (wapili kulia) akiwa na wanahabari wenzake enzi za uhai wake.

No comments:

Post a Comment