Monday, December 10, 2012

SHEREHE ZA MIAKA 51 YA UHURU WA TANGANYIKA KATIKA PICHA

Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wananchi wakati wa maadhimisho ya sherehe  za miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo. 
 Ngoma ya kitamaduni kutoka Zanzibar.
 Ngoma ya kitamaduni kutoka Rwanda
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakipita kwa mwendo wa haraka mbele ya Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete wakati wa maadhimisho ya sherehe  za miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo. 
 Askari wa Kikosi  cha majini akitolewa nje ya viwanja kwa ajili ya kupatiwa huduma ya kwanza baada ya kuishiwa nguvu
 Kikundi cha sanaa cha Taifa kutoka Rwanda kikitumbuiza katika sherehe hizo
 Wasanii wa kikundi cha Taifa kutoka Zanzibara wakitumbuiza kwa ngooma ya kitamaduni kutoka Pemba.
Askari wa Jeshi  la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakipita kwa mwendo wa haraka mbele ya Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete wakati wa maadhimisho ya sherehe  za miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo. 
 Watoto wa alaiki wakiwa katika gwaride la miaka 51 vya Uhuru wa Tanganyika zilizofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam
Watoto, Gozibety Mbwele (3) na Nyamburi Mganga (5) wa kikundi cha Utandawazoi kutoka Mwanza wakionesha manjonjo yako wakati wa sherehe za miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika zilizofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo. 
Vijana wa alaiki wakitengeneza maumbo ya vitabu.
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mama Maria Nyerere wakati wa maadhimisho ya miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika uliofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo. Chanzo Habari Mseto Blog

No comments:

Post a Comment