Monday, January 7, 2013

SIJATAPELI MOMBASA - PROFESA JAY

Prof Jay amethibitisha kuwa taarifa zinazo samba kwamba ametapeli Promoter Mombasa sio za kweli. Jay amesema alikubaliana na Promoter Eljah wa mjini Mombasa kuhusu show 2 ambazo zilikuwa tarehe 24 December iliyofanyika Jambori na Tarehe 25 Iliyofanyika Kwetu Beach. Show zote  Prof Jay alizifanya kama ilivyo pangwa ila Ilipofika muda wa kulipwa sasa hapo ndio tatizo lilipoanza.
Prof Jay


Prof Jay amekaririwa na sammisago.com akisema Promoter huyo alishindwa kumlipa pesa alizo takiwa kumlipa na kwa sasa Bado promoter huyo anadaiwa na Prof Jay Shilingi laki moja na Elfu Ishirini za Kenya [120,000] ambazo ni 2.201,215  Za Tz. Kila akipigiwa simu alikuwa anasema Jay nitakulipa baadae na halipi. Prof Jay amesema Promoter huyo hakulipa hata nauli yake ya kurudi Tanzania na Ilibidi Prof Jay aingie mfukoni na kulipia watu wake nauli na mambo mengine. Hizi ndio sababu zilizo mfanya jay asifanye show ya Tarehe 31 December iliyopangwa kufanyika  Jamboree.

Fahamu kuwa Mkataba wa makubaliano yao upo na promoter huyo aliandika pesa zote na makubaliano yao.Jay amesema anashangazwa sana na taarifa hizi kwani yeye ndiye anadai na sio kudaiwa chochote ndio maana promoter huyo ameongea hivyo kwenye vyombo vya habari ili kulinda jina lake. Pia alimaliza kwa kusema kabla taarifa kama hizi kusamba lazima waandishi wafanye uchunguzi kwani wanaweza kufanya watu kufikiriwa vibaya na jamii inayo wazunguka.




Hii Ndio Ilikuwa Post Ya Profesa Jay Kabla Ya Show Jamboree Mombasa.
Kwa hisani ya http://www.sammisago.com




No comments:

Post a Comment