Tuesday, September 11, 2012

Waandishi waandamana, Nchimbi atimuliwa







                        Dk Nchimbi akitolewa 'mkuku' katika maandamano hayo.





       Mhariri mtendaji wa C10 Dinna Chahali akitoa dukuduku lake leo.
                               Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri Tanzania,Nevil Meena akitoa Tamko.

"Kunawatu wanahoji tunaandamana alafu iweje wakati siye ndio wenye vyombo vya habari si  tuandike tu? Hapana kuandamana kwetu kunamaana sana tumeandamana sikama hatuna uwezo wakufanya kitu zaidi ya kuandamana, tunazo silaha kubwa zaidi ya maandamano lakini hii ni hatua ya pili baada ya matamko mbalimbali kutolewa.

Aidha Meena akahoji hivyo inakuaje kama sikumoja watu wakaamka wakakuta hakuna chombo chochote cha habari kilicho hewani hakuna tv, hakuna radio na wala hakuna magazeti nchi hii itakuwaje?

Wanahabari waendelee kuwa na utulivu hatua mbalimbali zitakazoendelea kuchukuliwa watafahamishwa kuhusiana na tukio hilo."

Viongozi wengi wa vyama vya waandishi wa habari waliotoa maoni yao kwenye mkusanyiko huo waliitaka serikali wachukue hatua na damu ya Mwangosi iwe shule kwao.

Katika tukio lingine, Waziri wa mambo ya ndani, Dk Emannuel Nchimbi alitimuliwa katika tukio hilo kwa kuwa hakutakiwa kuwa eneo hilo.

Dk Nchimbi alifika hapo kwa nia ya kutaka kuzungumza na waandishi hao kutoka vyombo mbalimbali vya habari, lakini hali ilikuwa tofauti baada ya kundi la waandishi hao kukataa kuhutubiwa na waziri Nchimbi.

Kukataa kuhutubiwa na Nchimbi kuliendelea na kuzomewa na kisha kusindikizwa na wapambe wake hadi katika eneo alilokuwa amepaki gari lake ambalo halikuwa na namba za waziri.

Maandamano hayo yaliyokuwa ya amani yalilindwa vyema na jeshi la polisi, pia yalikuwa ya nchi nzima yalihudhuriwa na idadi kubwa ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari.

Naye mhariri wa gazeti la Nipashe, Jesse Kwayu,"Sisi tunawalipa kodi polisi wapate sehemu za kuishi, bunduki, magwanda pamoja na buti na lengo ni kulinda raia na na mali zake na sio kuua watu, vitendo hivyi havivumiliki,".

No comments:

Post a Comment