Friday, September 14, 2012

Mkubwa Fella aibua vichwa kibaooo.....


Baadhi ya wasanii wanaounda kituo hicho chenye wasanii 37.

BAADA ya kuliongoza kwa mafanikio makubwa kundi nzima la TMK Wanaume family, meneja wa kundi hilo 'Mkubwa' Fella ameamua kuibuka tena safari hii akisaka vipaji ambayo havifahamiki kabisaaaa.

"Huku uswahili kuna vipaji si-vya kitoto, lakini wanapata tabu kwenda na kurudi studio matokeo yake wanaamua kukaa nyumbani na hatimaye vipaji hivyo vinakufa, lakini nimesikia kilio chao hapa Temeke mikoroshini nimefungua studio, nimefungua studio pamoja na kituo hiki kwa nia ya kuwaokoa wasanii wote wa huku chipukizi na hata wale maarufu ambao wengine walidondoka kimaisha na mimi nitawarekodia kwa mkataba na kuwa-manage," alisema Fella.

Alisema tangu kuanzishwa kituo hicho miaka kadhaa iliyopita tayari wasani kadhaa wameishaibuliwa akiwa Bibi Cheka pamoja na Dogo Aslay huku wasanii kibao dhaidi ya 37 wakiwa njiani kuibuliwa na kituo hicho wakiimba mchiriku, zouk pamoja na taarabu.


baadhi ya wasanii wa kike waliokuwemo kwenye kituo hicho.

No comments:

Post a Comment