Thursday, October 18, 2012

DIAMOND ATAMANI KUIRUDIA SHULE


WAKATI wasomi wengi wakisisitiza kuhusu vijana kutambua umuhimu wa elimu, msanii wa muziki wa muziki wa kizazi kipya, Nasseb Abdul ‘Diamond’, amedai kuwa anatamani kurudi shule kuendelea na masomo lakini kutokana na shughuli zake za muziki anakosa nafasi.

Akiongea na mwandishi wetu 
alidai kuwa anaamini elimu yake ya kidato cha nne ni ndogo sana na ana changamoto nyingi ili kufikia level za kimataifa, hivyo ana mipango ya kurudi shule lakini akifikilia mambo mengi muziki na ratiba za show huwa anakata tamaa kabisa lakini anaamini atafanya hivyo siku moja ili kutimiza ndoto yake ya kufika mbali zaidi kielimu.

Diamond
alisema kuwa kuna umuhimu wa yeye kwenda shule lakini kwa sasa hafikirii kama anaweza kukaa tena darasani na kumsikiliza mwalimu pengine aende nje kwa ajili ya kusomea muziki huku akiendelea na kazi hiyo hata huko atakapokuwa akisoma.

“Naweza kurudi shule lakini pengine nikasomee muziki na mambo mengine yanayohusu muziki,”
alidai.

No comments:

Post a Comment