Tuesday, October 30, 2012

SUMA LEE AIBIWA GARI

Kama utakuwa na kumbukumbu nzuri haina shaka kuwa utakuwa unakumbuka stori iliyochukua nafasi kwenye kipindi cha XXL siku chache zilizopita juu ya nyota wa songi la 'Hakunaga' Suma Lee kupata ajali wakati akiwa njiani kuelekea mkoani Kigoma kwa ajili ya kupiga shoo.
Taarifa kutoka Coco Beach zinasomeka kuwa nyota huyo mzaliwa wa mkoa wa Tanga ameibiwa ndinga yake hiyo aina ya Land Cruiser VX mwishoni mwa wiki iliyopita wakati alipokuwa kwenye mapumziko ya wikiend katika ufukwe wa bahari ya hindi.
"Haikuwa siku nzuri kwangu, nimeibiwa gari na watu ambao nahisi walikuwa wanaifuatilia kwa siku nyingi maana hata wakati wanaiba watu walikuwa karibu waliniambia kuwa watu hao hawakuvunja wala kuharibu chochote walichokifanya ni kufungua mlango kama ambavyo mimi huwa nafanya na kuwasha gari kisha kuondoka…"
Kama utakuwa na kumbukumbu nzuri haina shaka kuwa utakuwa unakumbuka stori iliyochukua nafasi kwenye kipindi cha XXL siku chache zilizopita juu ya nyota wa songi la 'Hakunaga' Suma Lee kupata jari wakati akiwa njiani kuelekea mkoani Kigoma kwa ajili ya kupiga shoo.
Hii ni gari ambayo inayofanana na gari aliyoibiwa Sumalee.

Taarifa kutoka Coco Beach zinasomeka kuwa nyota huyo mzaliwa wa mkoa wa Tanga ameibiwa ndinga yake hiyo aina ya Land Cruiser VX mwishoni mwa wiki iliyopita wakati alipokuwa kwenye mapumziko ya wikiend katika ufukwe wa bahari ya hindi.
"Haikuwa siku nzuri kwangu, nimeibiwa gari na watu ambao nahisi walikuwa wanaifuatilia kwa siku nyingi maana hata wakati wanaiba watu walikuwa karibu waliniambia kuwa watu hao hawakuvunja wala kuharibu chochote walichokifanya ni kufungua mlango kama ambavyo mimi huwa nafanya na kuwasha gari kisha kuondoka nalo kama la kwao," alisema Suma
Akiendelea zaidi Suma alisema kuwa kwa kuwa suala liko polisi hawezi kuzungumza sana ila ana uhakika gari yake ataipata tu kwani anafahamu watu wengi wanouza vifa avya magari Kariakoo labda kama watu hao wakiamua kulifugia kuku...alimaliza.

No comments:

Post a Comment